
Andengenye ameyasema hayo Jijini Dar es salaam na kusisitiza kwamba jeshi lake hupata wakati mgumu wakati wa matukio ya moto kwa baadhi ya watu kushindwa kupisha magfari hayo kwa kutojali yanakokimbilia.
''Ukiona gari la zimamoto jamani jaribu kuona kama ndiyo nyumba yako inaungua, fanya namna upishe gari hilo mara moja liwahi kwenye tukio likaokoe mali na nyumba''- Amesema Kamanda Andengenye.
Aidha Kamanda amewataka wananchi wanapojenga nyumba zao kuhakikisha wanaheshimu kuacha njia za kupita yanapotokea majanga ili magari yaweze kupenya kirahisi kufika maeneo yenye matatizo