
January Makamba
Kupiti ukurasa wake wa Twitter, Makamba amesema kuwa ameyapokea kwa moyo mweupe mabadiliko hayo na atakuwa katika nafasi nzuri ya kuzungumzia siku zijazo.
Kwa kweli nimeyapokea mabadiliko yaliyofanywa kwa moyo mweupe kabisa kabisa. Nitasema zaidi siku zijazo. pic.twitter.com/eXtOTtvYwQ
— January Makamba (@JMakamba) July 21, 2019
Nafasi yake sasa imechukuliwa na George Boniface Simbachawene. Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Hussein Mohamed Bashe, kuwa Naibu Waziri wa Kilimo. Bashe anachukua nafasi iliyoachwa na Mh. Innocent Bashungwa ambaye aliteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.