
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Hamisi Issah
Akizungumza leo Julai 16, kamanda wa Polisi mkoani humo, Hamis Issah amesema, tukio hilo limetokea Julai 15, baada ya watoto hao wenye umri kati ya miaka nane na kumi, kufanyiwa ukatili huo wakati wa mapumziko.
Kwa mujibu wa kamanda imeelezwa kuwa, watoto hao walitoroka shuleni na baada ya kurejea, mmoja wa wale watoto alikuwa anatembea huku akichechemea na baada ya kuhojiwa walidai wametoka kwa babu Yahya.
Na kwamba uchunguzi wa awali, umeonyesha watoto hao kubakwa, huku mmoja akiwa amelawatiwa.