Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Simba Hadji Manara akizungumza na waandishi wa habari
Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba Hadji Manara amesema haoni nafasi ya nyota Haruna Niyonzima kusajiliwa klabuni hapo licha ya kuwa yeye binafsi anamhusudu kwa uwezo wake.