Waliochoma makanisa Kagera wafungwa maisha
Mahakama ya hakimu mkazi Bukoba imewatia hatiani na kuwahukumu kifungo cha maisha watu watatu waliokuwa na tuhuma ya kuhusika na vitendo vilivyokuwa vimekithiri mkoani Kagera mwaka jana vya uchomaji wa makanisa katika maeneo mbali mbali mkoani humo.