Wanafunzi wa darasa la 7 waliofutiwa matokeo
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), limeyafuta matokeo ya watahiniwa 909, waliobainika kufanya udanganyifu katika Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi na kuagiza mamlaka kuwachukulia hatua, wale wote waliohusika kufanya udanganyifu katika mitihani hiyo.

