Naibu katibu Mkuu wa chama cha mpira wa wavu Tanzania (TAVA) Shukuru Ally amesema michezo ya mzunguko wa pili kwa upande wa Wanaume na Wanawake inataraji kuhitimishwa jumamosi ya wiki hii huku washindi wawili wa kila kundi watafuzu kushiriki hatua ya michezo ya Play Off .
"Mzunguko wa tatu ambao kutakuwa na mchezo wa mtoano utapigwa mwezi ujao pamoja na fainali ili tupate mshindi wa jumla'' Amesema Ally.
Kwa upande wao wachezaji wanaoshiriki mashindano hayo wamewapongeza TAVA kwa kurudisha ligi hiyo ambayo itachochea ushindani kwa vilabu na kuhamasisha watu wengi kujitokeza kucheza mchezo huo