Jumatatu , 7th Nov , 2016

TP Mazembe ya DR Congo imetwaa kwa mara ya kwanza, Kombe la Shirikisho Barani Afrika, baada ya kuifunga MO Bejaia 4-1, nyumbani.

 

Mchezaji wa kimataifa wa Zambia, Rainford Kalaba, alifunga mabao mawili, katika mchezo huo, ambao, ulikuwa wa marudiano baada ya kutoka 1-1 wiki iliyopita, mjini Blida.

Mazembe imeshinda kwa jumla ya mabao 5-2, na hili ni taji lao la pili mfululizo katika mashindano ya Afrika, baada ya mwaka uliopita kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa.