Ijumaa , 25th Mei , 2018

Mbuzi 47 wenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni mbili mali ya bwana Sleyo Rashidi mkazi wa mjini Shinyanga, wamedaiwa kufa kwa kula majani yenye sumu katika eneo la marisho Jeshini Kata ya Kizumbi mjini hapa, sehemu ambayo mbuzi hao walikuwa wakichunga. 

Imedaiwa mbuzi hao waliaanza kufa usiku wa kuamkia leo Mei 25,2018 katika kitongoji cha Busongo Kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi majira ya saa 10 usiku, ambapo sumu hiyo waliokula kutoka machungoni eneo hilo la Jeshi, ilianza kuwazidi na kuanza kufa mmoja baada ya mwingine. 

Akisimulia tukio hilo mchungaji wa mifugo hiyo Daudi Dotto, amesema ilipofika majira ya saa 10 usiku alianza kusikia mbuzi wakilia, na alipo kwenda kwenye banda lao alikutana na mbwa huku mbuzi 47 wakiwa wameshakufa na matumbo yao kuvimba. 

“Mbuzi hawa hua na wachunga mara zote katika eneo la Jeshini Kizumbi ambapo hua tunakatazwa, lakini kutokana na uhaba wa maeneo ya marisho hua tunachunga hivyo hivyo kwa kuiba , na majira ya jioni ni kazirudisha nyumbani  ndipo majira hayo ya usiku wakafa mbuzi 47,” amesema Dotto. 

Naye Daktari wa mifugo wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Velani Mwaluko ambaye alifika kwenye eneo hilo, alisema katika uchunguzi wa awali amebaini mbuzi hao wamekufa  kwa kula majani yaliyopuliziwa Sumu, ambapo amechukua baadhi ya Nyama kwenda maabara Jijini Mwanza, ili kubaini aina hiyo ya Sumu.