Jumanne , 12th Oct , 2021

Timu ya Ujerumani imekuwa timu ya kwanza kufuzu kushiriki kombe la dunia linalotaraji kufanyika nchini Qatar mwaka 2022 baada ya kupata ushindi wa magoli 4 kwa bila  dhidi ya timu ya North Macedonia kutoka kundi J.

Wachezaji wa Ujerumani wakishangilia moja ya bao walilofunga dhidi ya Northen Macedonia.

Magoli mawili ya mshambuliaji Timo Werner, Kai Havertz na Jamal Musiala  yametosha kuwapa nafasi Ujerumani tiketi ya kushiriki michuano hiyo mikubwa duniani baada ya kufikisha alama 21 huku akisaliwa na michezo miwili  dhidi ya Liechtenstein nyumbani mwezi November na ugenini dhidi ya Armenia.

Baada ya kuwavusha Ujerumani, Kocha Hansi Flick atakuwa na kibarua pevu cha  kusaka mafanikio zaidi kwa taifa hilo baada ya miaka 15 ya mtangulizi wake Joachim Low kuwapa kombe la dunia mwaka 2014 nchini brazil na kombe la mabara mwaka 2017 nchini Urusi.

Hii itakuwa mara ya 20 kwa taifa la Ujerumani kushiriki kombe la dunia wakiwa nyuma ya  Brazil ambao wameshiriki mara 21 huku Ujerumani wanarudi wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kuondoshwa kwenye hatua za makundi kama bingwa mtetezi mwaka 2018 nchini Urusi.