Jumatano , 23rd Jun , 2021

Mwimbaji wa muziki kutoka Nigeria, Teni amevunjika mkono wake wa kulia wakati akitayarisha video ya wimbo mpya kutoka kwenye album yake ‘Wondaland’ aliyoiachia hivi karibuni.

Picha ya Msanii Teni

Hit maker huyo wa ‘Billionaire’ ame-share picha na video (BTS)  za matukio mbalimbali wakati akitayarisha video hiyo ambapo ameonekana akiwa kwenye kiti cha mbele cha gari lililokuwa limening’inizwa hewani huku yeye akiimba wimbo ambao walikuwa wakiufanyia video.

Album ‘Wondaland’ ilitoka Machi 19, 2021 huku ikiwa na nyimbo 17 na collabo moja pekee kutoka kwa msanii mwenzie wa Nigeria Davido.