Jumanne , 19th Sep , 2017

Msanii wa bongo fleva na mama wa mtoto mmoja Linah Sanga ameibuka na kusema akibeba mimba nyingine hataacha kupiga picha zake tata kama  alizozipiga kipindi akiwa na mimba yake ya kwanza kwa kuwa yeyeni mtu maarufu.

Akiongea kupitia eNewz Linah amesema hajutii kwa picha alizozipiga katika kipindi  cha ujauzito wake wakwanza kwa kuwa yeye ni mtu maarufu  na aliamua kufanya kitu ambacho roho yake ilijisikia kufanya kwa kipindi kile na kuongeza kwamba  hata siku akibeba mimba nyingine anaweza kufanya kitu kama hicho kwa kuwa hakikumuharibia chochote katika maisha yake.

Hata hivyo  Lina aliendelea kusema kwamba "Binadamu ni watu wa ajabu sana na hata ufanye nini huwezi kuwaridhisha kwa kuwa kila mtu anatamani ufanye kile anachokitaka yeye nikivaa gauni refu watasema mimi nimshamba na hata nimevaa hizo nguo fupi bado wanasema hazina maadili hivyo mi nafanya ninachojisikia na waacha waendelee na malumbano yao"alifunguka mbele ya kamera za eNewz

Mbali na hayo Linah amefafanua pia suala la watu kumuona yeye kama amechelewa kujifungua ni kutokana na kwamba watu wengi  waliwahi kufahamu hali yake mapema tangu ikiwa na miezi mitatu hivyo walikuwa kama wanamuhesabia na ilipopitiliza wiki ndipo walipoanza kuhoji.