Ijumaa , 6th Mei , 2022

Rapa Country Weezy ameeleza kuna figisu ambazo anaona anafanyiwa na baadhi ya watu wasiomtakia mema kwa kutaka kuhack akaunti yake ya Instagram na Youtube.

Picha ya Country Wizzy

Country Weezy ameshea ujumbe huo unaoeleza kwamba 

"Its almost a week naona account yangu ya Youtube kuna Raia kwa hisia zao binafsi wanajaribu ku-hack, kwanza nilifika views laki 300k in 3 days, Baada ya hapo views wakaanza kupungua".

"Kuna mkono wa mtu unaendelea, sio tu youtube mpaka instagram naona mkono wa mtu unavoendelea. Nasisitiza kama kijana niliejiajiri kupitia Sanaa yangu Nakemea na ninalaani kitendo hichi kinachoendelea Tufanyeni kazi kama Serikali yetu inavosisitiza".