Jumatano , 12th Mei , 2021

Rapper Soulja Boy anakabiliwa na kesi ya ukatili na unyanyasaji wa kingono, vitendo hivyo alimfanyia mwanamke wake wa zamani (Ex) na kumsababishia ujauzito kuharibika.

Msanii Soulja Boy

Kwenye documents za Mahakama kuu zilizodakwa Jumanne huko Los Angeles na mtu ambaye hakujitambulisha jina lake, amesema kuwa Rapper huyo alianza kumpiga ngumi Ex wake, zilimfanya aanguke chini ambapo aliukunja mwili ili kulinda tumbo lake na kutumia mikono kufunika kichwa sehemu za uso baada ya kukasirika wakati wa mazungumzo mnamo 2015.

Katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2019, Soulja amefanya matukio ya kikatili kwa wanawake kadhaa na wakili Neama Rahmani anasema ni suala la muda tu kwa Soulja boy kukamatwa kabla hajamtoa uhai mmoja wa athirika.