Alhamisi , 18th Mei , 2017

Mmiliki wa Shule, Meya wa jiji la Arusha pamoja na waandishi wa habari 10 wamefikishwa kituo cha polisi (Central) kwa kufanya mkusanyiko bila kibali ndani ya shule ya Lucky Vicent.

Kutoka Arusha taarifa zinasema kuwa Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Arusha (jina lake halijafahamika) amedai kuwa kosa ambalo wamelifanya waandishi pamoja Wamiliki ni kufanya mkusanyiko bila kibali ambao ni kinyume cha sheria.

Vyanzo vya habari vinadai kuwa chanzo cha kukamatwa ni baada Wamiliki wa shule binafsi kwenda shuleni Lucky Vicent kutoa michango ya Rambirambi shuleni Lucky Vicent

Habari zinasema kuwa kwa sasa Watu wote waliokamatwa tayari wamefikisha kituo cha kati kilichopo mjini Arusha (Central)
Waliokamatwa kwenye msafara huo wanatajwa ni wanahabari 10, Mmiliki wa shule ya Lucky Vicent na Meya Kalist Lazaro.

Waandishi waliokamatwa ni pamoja na  1 .Godfrey Thomas ayo tv 2.Alphonce kusaga Triple A 3.Filbert Rweyemamu mwananchi 4.Husein Tuta Itv 5.Joseph Ngilisho Sunrise radio 6.Geofrey Steven Radio 5 7.Janeth Mushi Mtanzania 8.Zephania Ubwani The Citizen 9.Elihuruma Yohani mwakilishi wa Tanzania Daima 10.Idd uwesu Azam Tv