Jumatano , 23rd Mei , 2018

Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Musukuma, amesema kwamba watu wanaomsema Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kuhusu watu wasiojulikana na wanao likashifu jeshi la polisi na kulituhumu kwa mambo yasiyofaa wanalikosea jeshi hilo, kwani bila wao tusingekuwa salama.

Musukuma ameyasema hayo alipokuwa KIKAANGONI  East Africa Television, na kusema kwamba iwapo jeshi la polisi likiacha kazi kufanya kazi hata kwa siku moja hakutakuwa na amani, kwani watu watafikia hatua ya kubakana bila kutongozana.

“Ilitengenezwa tu chuki kuwa watu wasiojulikana wanatumwa na Makonda, sijui na nani!! Mara polisi, hii dhana si nzuri, haya matukio yametokea sehemu nyingi, Kibiti huko, sijui wapi huko, ila mnalichafua tu jeshi la polisi , Siku jeshi la Polisi likisema liache kufanya kazi, hali itakuwa mbaya, hatutatongozana tutabakana.”, amesema Musukuma.

Sambamba na hilo Musukuma amesema watu wanaofanya hivyo hawako sahihi, kwani badala yake wanapaswa kulishukuru jeshi hilo kwa jukumu la kuwalinda wao na mali zao.