Matofali
Kero hiyo pia imetolewa na wakazi wa Kata hiyo hasa wanaume, jambo linalowaumiza zaidi pindi wake zao wanapoenda kliniki kujua maendeleo ya afya zao, badala ya kuwapa huduma za kitabibu wanawapa adhabu za kufagia na kusomba tofali.
Akijibu malalamiko ya wananchi hao Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu, amewataka wahudumu wa afya wa kituo hicho kuzingatia maadili ya kazi yao na kuacha mara moja tabia ya kuwafanyisha kazi wagonjwa na kuwanyanyasa.