Jumatatu , 15th Nov , 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amewatakia kheri wanafunzi wote wanaoanza mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne hii leo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Kupitia ujumbe wake aliouandika hii leo Novemba 15, 2021, kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Samia amesema serikali inaendelea kujenga nafasi zaidi kwenye nyanja mbalimbali yakiwemo mazingira bora ya ajira.

"Nawatakia kila la kheri wanafunzi wote wa kidato cha nne wanaoanza mitihani yao leo, tunaendelea kujenga nafasi zaidi kwao kusonga mbele kielimu, kiujuzi na kiajira, kwa kuongeza nafasi za kidato cha tano na sita, vyuo vya ufundi stadi na mazingira bora ya nafasi zaidi za ajira," ameandika Rais Samia.