Msemaji wa Jeshi la Polisi SACP David Misime,
Msemaji wa Jeshi la Polisi SACP David Misime, amesema kuwa licha ya tahadhari hiyo lakini hali ya ulinzi na usalama hapa nchini ni shwari na kwamba matukio makubwa yanayoweza kuleta hofu kwa wananchi yanaendelea kudhibitiwa.
Taarifa iliyotolewa jana Januari 25, 2023 na Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania
Aidha SACP Misime amesema kwamba pale itakapobainika uwepo wa jambo au watu wenye kutia shaka kutokana na mienendo yao taarifa zitolewe haraka ili ziweze kufanyiwa kazi.