Ijumaa , 25th Mei , 2018

Serikali ya Uganda inatarajiwa kuanza kulipa mishahara ya watumishi wake wa umma kulingana na siku walizofanya kazi badala ya hakikisho la mshahara wa mwisho wa mwezi.

Mkuu wa Kitengo cha Uwajibikaji cha Ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Prof. Ezra Suruma amesema wameanza kufunga vifaa vya kielektroniki ambavyo vitafuatilia muda wa kuingia na kutoka kazini kwa watumishi wa umma kwenye hospitali zote za umma na taasisi za elimu.

"Mishahara ya wafanyakazi ambao hawatahudhuria kazini bila sababu maalum itakatwa kulingana na siku ambazo hawakufanya kazi", amesema Prof. Suruma

Prof. Suruma amefafanua zaidi kuwa mfumo huo tayari umeanza kutekelezwa katika Wilaya za Kaliro, Kayunga, Buvuma, Bulambuli, Bugiri na Bududa, Mashariki mwa Uganda kwa majaribio na kwamba wanatarajia utaanza katika Wilaya zote nchini humo