Kamishna Msaidizi wa Uchambuzi wa Sera kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, William Mhoja
Hayo yamebainishwa leo na Kamishna Msaidizi wa Uchambuzi wa Sera kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, William Mhoja wakati akitoa ufafanuzi kufuatia kauli ya Waziri wa fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba kuhusu hatua zilizochukuliwa na serikali katika miamala hiyo.
Mhoja amesema kuwa serikali inakusudia pia kusamehe tozo za miamala kuanzia Shilingi 0 hadi 30,000 kwa huduma zote za miamala ya fedha ambapo vyote vitawekwa bayana kwenye kanuni baada yakukamilika na kuanza kutumika Oktoba 1, 2022.