William Ruto, Mteule Urais nchini Kenya
Matokeo hayo yametangazwa hii leo Agosti 15, 2022, na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya (IEBC), Wafula Chebukati, na kusema Ruto amepata zaidi ya kura milioni 7 akifuatiwa na mshindani wake Raila Odinga, aliyepata zaidi ya kura milioni 6.
Matokeo ya Urais nchini Kenya yametangazwa wakati ambao, Tume ya IEBC ikiwa imegawanyika kwa baadhi ya maafisa wa tume hiyo.