
Mwenyekiti wa chama cha UDP, Mzee John Cheyo.
Mzee Cheyo ametoa kauli hiyo hii leo Julai 24, 2020, wakati akizungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio.
"Nakumbuka mwaka 2000 tukiwa kwenye kampeni Mwanza, gari lake liligonga watu na kwa bahati mbaya walifariki, nilienda kumfariji nikamkuta anatoa machozi kuwalilia wale watu, alikuwa ni mkali lakini alikuwa na moyo wa kuhurumia watu" amesema Mzee Cheyo.
Aidha Mzee Cheyo ameongeza kuwa, "Kwangu Mkapa ni kiongozi aliyekuwa na busara, kama kulikuwa na mtu ambaye alikuwa anatoa hotuba mpaka zina kusisimua na kama kulikuwa na kiongozi aliyetumia lugha ya Kiingereza vizuri ni Mzee Mkapa".
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo Julai 24, 2020, katika moja ya Hospitali zilizopo jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.