Mwenge wa Uhuru
Taarifa hiyo imetolewa Visiwani Zanzibar ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi, Mei 17 mwaka huu anatarajiwa kuzindua mbio hizo kitaifa katika uwanja wa Mwehe, Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja.
Ambapo baada ya uzinduzi huo Mwenge wa Uhuru utaanza mbio zake chini ya vijana shupavu sita kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ), kwa siku 150.