Polisi wameongeza kuwa wanaendelea kuwasaka watu wengine kuhusiana na mauaji hayo.
Mauaji ya David Sunday Imoh mwenye umri wa miaka 38 yameleta mdahalo mkubwa kwenye mitandao ya kijamii nchini Nigeria huku kukiwa na hashtag isemayo #JusticeForDave ikitapakaa kwenye mitandao ya kijamii.
Hakuna sababu zilizobainishwa juu ya mauaji ya kijana huyo ambaye alipigwa kama mwizi na kisha kuchomwa moto.
Lakini kumekuwa na madai mitandaoni kwamba , yalitokea majibizano baina na David na mwendesha bodaboda juu ya malipo ya safari baada ya kufikishwa kwenye club ambapo ndio kazini kwake.
Mauaji haya yanatokea katika kipindi ambacho Wanaigeria wanaendeleza taharuki juu ya mauaji ya mwanafunzi wa kike huko kaskazini mwa jiji la Sokoto ambaye aliuawa kwa sababu ya kuikashifu imani ya kiislamu.