Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, akizungumza na IGP Camillius Wambura
Kauli hiyo ameitoa hii leo Agosti 18, 2022, alipokutana na kufanya mazungumzo na na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillius Wambura, na kulitaka jeshi la polisi kutenda haki pasipo kuonea mtu yeyote na yeyote anayevunja sheria achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria na sio vinginevyo.
Katika mazungumzo hayo, Makamu wa Rais amelipongeza jeshi la polisi kwa kuendelea kuimarisha amani pamoja na ulinzi wa wananchi na mali zao.