Makamishna hao wanadai Mwenyekiti, Wafula Chebukati, aliwapindua na kusisitiza kutangaza matokeo licha ya wao kuwa na wasiwasi juu ya matokeo hayo
Aidha wanadai kuwa kuwa hesabu ya mwisho ya matokeo ya uchaguzi wa urais haikuletwa mbele ya tume ili kushughulikiwa.
Sababu nyingine walizoeleza wamesema kuwa kuwa ujumlishaji wa matokeo haukuwa sahihi kimahesabu na kwamba matokeo hayo hayajumuishi jumla ya waliojiandikisha kupiga kura na kura zilizopigwa au zilizokataliwa
Tayari Raila Odinga ametangaza kuyakataa matokeo hayo leo