Alhamisi , 29th Sep , 2022

Baadhi ya wachumi, watafiti nguli pamoja wakazi katika Jiji la Dar es Salaam wamesema changamoto kubwa ya ukuaji wa miji ni uhamiaji watu kutoka vijijini kuja mijini wakitaraji kupata uchumi imara hali inayochangia makazi holela.

Changamoto ya makazi holela

Hata hivyo mtaalam wa mipango miji ambaye pia amehudumu kama Mkurugenzi wa Nyumba Wizara ya nyumba na makazi Kwa kipindi kirefu     Prof Tumsifu Nkya ameeleza kuwa jambo muhimu kwenye upangaji wa miji ni takwimu sahihi za idadi ya watu kwenye Mji husika Ili kuepuka uholela unaojitokeza Kwa sasa.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji na mtafiti nguli kutoka taasisi ya utafiti ya Repoa dkt Donald Mmari amesema kufikia mwaka 2030 Jiji la Dar es Salaam litakuwa ni miongoni mwa majiji makubwa Africa hivyo ni lazima sasa kulipanga upya Kwa mliangano sawa wa watu na mifumo ya huduma za jamii zitakazolinda utunzaji wa mazingira.

"Kwa sasa kasi ya ukuaji na upangaji wa miji ni ndogo kuliko kasi ya watu kuingia mijini hivyo ni wajibu wa taasisi za serikali wadau kuja na mpango kazi maalum na ndo maana tunafanya tafiti ili kuja saidia sera"alisema dkt Donald Mmari

Matarajio ya Watanzania wengi yameonesha Imani na unafuu mkubwa kiuchumi mijini tofauti na ilivyo vijijini Hali inayopelekea eneo Moja watu kuhamia Kwa wingi hivyo kusisitizwa uwekezaji  wa kasi kwenye mipango miji hapa Tanzania.