Katika uchaguzi huo uliofanyika jana Oktoba 9, 2021 Cherehani alipata kura 103,357 dhidi ya mshindani wake Bw. Mabula Nkwabi Julius wa ACT Wazalendo aliyepata kura 3,588 kati ya kura 106,945 zilizopigwa.
Uchaguzi huo umefanyika kufuatia aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Elias John Kwandikwa ambaye pia alikuwa Waziri wa Ulinzi kufariki Agosti 2, 2021.