Jumatano , 22nd Nov , 2017

Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA, leo limetangaza majina ya wachezaji 50 wanaowania kuingia kwenye kikosi cha wachezaji 11 bora mwaka 2017.

Kikosi hicho kimejumuisha wachezaji kutoka vilabu mbalimbali ambao wamefanya vizuri mwaka huu. Waliotajwa ni makipa Gianluigi Buffon, David De Gea, Keylor Navas, Manuel Neuer na Jan Oblak.

Walinzi waliotajwa ni Dan Alves, Bonucci, Carvajal, Chiellini, Camil Glik, Goddin, Kimmich, Marcelo, Mendy, Meunier, Pique, Ramos, Sanchez, Sandro na Valencia.

Kwa upande wa viungo ni Delle Alli, Ansensio, Casemiro, De Bruyne, Eriksen, Fabinho, Hazard, Iniesta, Isco, Kroos, Modric, Mkitharyan, Pyanic, Pogba, na Saul Niguez.

Wengine ni washambuliaji Karim Benzema, Aubamayeng, Aguero, Cavani, Dybala, Falcao, Griezman, Kane, Lewandowski, Mbappe, Mertenes, Messi, Neymar, Ronaldo na Suarez.