Jumatatu , 25th Sep , 2017

Shirikisho la soka nchini TFF, leo Septemba 25 limesaini mkataba na benki ya KCB wenye thamani ya shilingi 325,000,000.

Akiongea wakati wa kusaini mkataba huo Rais wa TFF Wallace Karia amesema huo ni ushahidi kuwa shirikisho lina ushirikiano na wadau mbalimbali wa mpira nchini.

Aidha Karia amesema fedha hizo zitaelekezwa kwenye kukuza vipaji vya soka pamoja na maendeleo ya soka nchini kwa ujumla.

Huu ni mkataba mkubwa wa kwanza kusainiwa na shirikisho hilo tangu uongozi mpya chini ya Rais Wallace Karia uingie madarakani August 12 mwaka huu.