Picha ya Mascot wa klabu ya Simba
Akieleza leo mbele ya waandishi wa Habari, Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzales amesema, Mascot hao watakuwa wakihudhuria mechi za Simba popote nchini kuanzia kwenye tamasha la Simba Day mwaka huu lakini pia watatumika kujenga ukaribu na kuwahamasisha watoto kupenda mchezo wa mpira.
Simba itacheza mchezo wa kirafiki na klabu ya TP Mazembe kutoka jiji la Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kwenye kilele cha maadhimisho ya Simba Day Septemba 19 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa