Jumatano , 19th Jan , 2022

Klabu ya soka ya Simba SC imeeleza kupokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha shabiki wake Khalfan Mwambena, ambaye kwa mujibu kwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Christina Musyani alijinyonga Jumatatu Januari 17, 2022.

Nembo ya Simba SC

Taarifa hiyo imefafanua kuwa marehemu Khalfan alijinyonga kabla ya mechi ya Mbeya City vs Simba SC ambao uliisha kwa Simba SC kupoteza 1-0.

Soma zaidi taarifa ya klabu ya Simba SC.