Jumapili , 15th Jan , 2017

Everton imepeleka msiba mzito kwa kocha Pep Guardiola baada ya kuifunga Manchester City mabao 4-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza.

Kocha wa Man City Pep Guardiola, alikuw akiona kama ndoto hivi

Romelu Lukak, Kevin Mirallas walifunga mabao kipindi cha kwanza na kuipeleka Everton, kuongoza, mbele ya City, iliyokuwa imetawala mchezo kwa 71 asilimia.

Tom Davies aliwainua tena wapenzi wa uwanja wa Goodison Park kwa kumtungua kipa wa City, Claudio Bravo na Ademola Lookman alifunga bao la 4, kwenye dakika za majeruhi, na kuwaacha matajiri wa Manchester, wakitoka patupu.

Machester City, sasa inakaa nafasi ya tano ikiwa na pointi 40 baada ya michezo 22.

Hiki ni kipigo cha kwanza kikubwa cha aina hiyo kwa kocha wa Man City Pep Guardiola tangu aanze kufundisha soka la ushindani

Ademola Lookman, akipongezwa na kocha wake Ronald Koeman baada ya kufunga bao kwenye mechi yake ya kwanza dhidi ya Man City

Katika mchezo mwingine uliowakutanisha watani wa jadi Manchester United na Liverpool, matokeo yameuwa ni sare ya bao 1-1 ambapo wageni Liverpool ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 27 kupitia kwa James Milner kwa mkwaju wa penati, kabla ya Zlatan Ibrahimovic kusawazisha kwa kichwa dakika ya 83.