Jumatatu , 13th Feb , 2017

Bingwa wa dunia wa mkanda wa WBO uzito wa welterweight, Manny Pacquiao amewaomba mashabiki wake wa kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter kumchagulia bondia wa kupambana naye katika mchezo ujao.

Manny Pacquiao

Mabondia hao ni Amir Khan na Kell Brook, wa Uingereza, Jeff Horn wa Australia na Terence Crawford, wa Marekani.

Pacquiao amesema pambano hilo la kutetea mkanda ambao alishinda katika mwezi wa Novemba mwaka uliopita, litafanyika katika nchi za falme za kiarabu.

Mfilipino huyo mwenye umri wa miaka 38, na bingwa mara 6 wa dunia, alitangaza kustaafu katika mwezi wa Aprili, mwaka uliopita, lakini alirejea tena ulingoni na kumshinda Jessie Vargas mwezi wa Novemba, mwaka jana.