Jumatatu , 21st Sep , 2020

Lamine Moro, beki kisiki wa Yanga amesema kuwa mpango mkubwa wa timu hiyo ni kuwa na mwendelezo mzuri katika mechi zao zote ndani ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21.

Beki wa Yanga, Lamine Moro (Kushoto) akiwa na mshambuliaji wa zamani wa Timu hiyo Sadney Urikhob (Kulia) kwa pamoja walipokua mazoezini.

Beki huyo amesema "Kikubwa tunahitaji sapoti kutoka kwa mashabiki ili tuweze kuendelea kuwa bora kwani sapoti yao ni muhimu kwetu katika mchezo yoyote"

kwa upande mwingine beki huyo amesema mchezo unaofuata kwa dhidi Mtibwa Sugar ni mchezo mgumu kutokana na timu nyingi za mikoani pindi zinapokutana na timu za Yanga na Simba waga zinakamia kwaajili ya kupata matokeo mazuri.

''Tuna waheshimu sana Mtibwa kutokana na ubora ambao walionyesha katika mechi zao lakini sisi tutaingia uwanjani kucheza kwaajili ya kupata matokeo mazuri '' amesema Lamine Moro.

Kikosi cha Yanga kimerejea Dar es salaam baada ya kushinda mchezo dhidi ya Kagera Sugar, Septemba 19 bao 1-0.bao pekee la ushindi lilifungwa na Tonombe Mukoko dakika ya 72 baada ya mabeki wa Kagera Sugar kushindwa kuokoa hatari iliyopigwa na Tuisila Kisinda.

Yanga ipo nafasi ya tatu nyumba ya vinara Azam wenye alama 9, huku  watani zao wekundu wa msimbazi Simba wakiwa nafas ya pili wakiwa na alama 7.