Haji Manara
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu, Jerome Msemwa amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya Manara kukutwa na makosa matatu dhidi ya TFF ambao ni walalamikaji.
Makosa hayo ya Manara dhidi ya mlalamikaji TFF ni kuituhumu na kuidhalilisha TFF, kueneza chuki za ukabila na la tatu kuingilia utendaji wa shirikisho hilo.
Siku chache zilizopita Manara aliituhumu TFF kufanya njama za waziwazi ili kuwabeba wapinzani wao Yanga kwenye Ligi Kuu.
Manara pia aliwatuhumu viongozi wakuu wa TFF, Jamal Malinzi na Katibu wake, Selestine Mwesigwa ni wahaya na viongozi wa zamani wa Yanga, ambao wanataka kuipendelea Kagera Sugar.