Jumanne , 23rd Mei , 2017

Katibu mkuu wa Mabingwa Ligi Kuu Tanzania Bara Young Africans, Charles Boniface Mkwasa ameweka wazi mipango yao kuwa kusema wanatarajia kupeleka kombe lao bungeni kwa lengo la kuwapa fursa wabunge pamoja na wanachama wake kuliona.

Katibu mkuu Yanga, Charles Boniface Mkwasa

Mkwasa amebainisha hayo katika taarifa aliyoitoa leo kwa kusema  walipanga kucheza mechi moja katika uwanja wa Jamhuri uliopo Dodoma, lakini imeshindikana hivyo wataamishia mchezo huo katika jiji la Arusha.

"Tumeweka mipango yetu vizuri tutalipeleka kombe letu Dodoma ili wanachama wetu na wabunge wenye mapenzi na Yanga SC walione kombe letu ambalo tumelichukua mara tatu mfululizo. Tulipanga kucheza mechi moja Dodoma lakini uwanja umefungwa hivyo tutawaonesha na kuondoka kuelekea jijini Arusha....Ukiachilia mbali mikoa hiyo miwili msafara wa Yanga utajitahidi popote unapokatisha kusimama kidogo kuwaonesha wanachama wake kombe lao ili kufurahia juhudi na kazi". Alisema Mkwasa

Yanga inatarajia kucheza mchezo huo wa kirafiki mwishoni mwa juma hili.