Nyota wa Yanga, Carlinhos Carmo atakayeukosa mchezo wa kesho dhidi ya KMC kutokana na kuwa na adhabu ya kadi nyekundu.
Wachezaji watakaokosekana ni viungo Haruna Niyonzima aliyewasili nchini jana akitokea kwenye kambi ya timu yake ya taifa ya Rwanda, Carlinhos anayetumikia adhabu ya kuoneshwa kadi nyekundu wakati Mapinduzi Balama na Mlinzi wa kushoto Yassin Mustapha wanauguza majeraha yao.
Pia amethibitisha kuwa mshambuliaji Said Ntibazonkiza amerejea kikosini baada ya kuwa nje kutokana na majeraha.
Ligi kuu soka Tanzania imerejea katika mwendelezo wake ambapo Yanga itakuwa inacheza mchezo wake wa 24 ikiwa inaongoza ligi kwa pointi 50. KMC wao wapo nafasi ya 5 wakiwa na pointi 35 kwenye mechi 24.