Akizungumzia mchezo huo Kocha Mkuu Aristica Cioaba amesema wamejipanga vizuri katika kuhakikisha wanachukua alama tatu katika mechi yao ya leo japo kuwa anatambua kila timu inawachezaji wazuri.
"Ninafuraha sana kuona wachezaji wanafanya mazoezi kwa nguvu na kusikiliza kila ninachotaka katika mechi hii dhidi ya Lipuli. Napenda kusema naheshimu kila timu hapa Tanzania kwa kuwa kila mmoja ana wachezaji wazuri lakini mipango yetu kwa leo ni kucheza soka zuri na kuchukua pointi tatu", alisema Cioaba.
Azam FC inashuka dimbani ikiwa na alama saba kibindoni ikiwa nyuma kwa pointi mbili alizokuwa nazo Mtibwa Sugar mpaka hivi sasa, ambapo naye Mtibwa Sugar atakuwa dimbani siku ya leo dhidi ya Ruvu Shooting FC akisaka alama tatu huku akimuombea njaa Azam FC asifunge ili aweze kubakia yeye nafasi ya juu.