Jumatatu , 20th Mar , 2017

Klabu ya soka ya Arsenal imekanusha taarifa zilizotoka Ujerumani, kuwa imeongea na kocha wa Borussia Dortmund, Thomas Tuchel awe mbadala wa kocha wa timu hiyo, Arsene Wenger.

Thomas Tuchel - Kocha wa Dortmund

Msemaji wa klbu hiyo, amesema taarifa za gazeti moja la nchini Ujerumani ni uongo, na swala la kuachana na Wenger litakuwa katika mchakato maalumu, na kwa sababu za msingi.

Wenger kwa miezi kadhaa amekuwa akisakamwa na mashabiki wa klabu hiyo, kuwa aondoke, kutokana na timu hiyo, kukosa mataji kwa muda mrefu.

Arsenal, hivi karibuni imetolewa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Barani Ulaya, na hadi sasa inakalia kuti kavu la kumaliza nne bora kwenye ligi ya EPL, baada ya Jumamosi kufungwa 3-1 na West Brom, na kujikuta wakishuka hadi nafasi ya 6.