Jumapili , 15th Jan , 2017

Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2017) imeanza usiku wa jana kwa kushuhudia sare mbili ikiwemo ya mwenyeji Gabon ambaye amelazimishwa sare ya bao 1-1 na Guinea Bissau katika mchezo wa ufunguzi

Burkina Faso vs Cameroon

Guinea Bissau walisawazisha bao la Aubameyang lililofungwa dakika ya 51 kunako dakika ya 89 kupitia Soares

Katika mchezo wa pili, Cameroon pia imelazimishwa sare ya bao 1-1 na Burkina Faso.

Leo zinapigwa mechi mbili ya kundi B, ambapo saa 1:00 jioni Algeria inakipiga na Zimbabwe huku Tunisia ikikipiga na Senegal saa 4:00 Usiku.

Haya ndiyo makundi