Jumatano , 25th Mei , 2022

Kipaji ni kitu ambacho watu wengi wamejaaliwa kuwa nacho ila ni watu wachache huwa wanafanikiwa kugundua vipaji vyao nakuvifanyia kazi mpaka wanafanikiwa

Ochieng hakuwahi kusomea ufundi wa magari

Kijana mmoja kutoka Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya anayetambulika kwa jina la Bernard Otieno Ochieng, ameshangaza watu kutokana na kipaji chake na uwezo wa ubunifu baada ya kubuni gari lake la siti mbili za kukaa.

Mwaka 2010, Ochieng aliacha shule baada ya kushindwa kulipa karo, baada ya hapo alianza kujifunza ufundi wa magari kwa sababu ni kitu ambacho alikuwa anakipenda tangu akiwa shule. Kipindi yupo shule alikuwa anapenda kutumia computer kuangalia mtandaoni jinsi magari yanavyoundwa na kujifunza.