Jumamosi , 27th Mei , 2017

Muongozaji wa video za muziki wa bongo, Nisher amefunguka kufafanua kwa nini amekuwa akitumia rangi nyeusi katika kazi zake na kudai ni ubunifu wa kujitofautisha na watu wengine wengi wanaofanya kazi hiyo.

Muongozaji wa video, Nisher

Nisher amefunguka hayo baada ya maswali mengi mtaani kuzagaa kwa kipindi kirefu  kwa nini anatumia rangi nyeusi, kwa kudai kwamba video ni kama nguo ikivaliwa leo kesho itapumzishwa hivyo yeye kuweka rangi nyeusi ni kubadilisha mionekano ya rangi za video kama ilivyokuwa imezoeleka hapo awali.

Picha ya  wimbo wa weusi 'Gere' aliouongoza Nisher.

Aidha Nisher amefafanua na kusema kwamba  elimu ya uongozaji wa videoi aliyoipata nchini Marekani inamsaidia sana katika kufanya kazi zake kitaalamu jambo ambalo lilimfanya wasanii wengi kumkimbilia tangu alipojiingiza kwenye tansnia ya muziki.

"Kutumia elimu kwenye tasnia ya video ni nzur kwa sababu inakufanya uwe smart kuanzia kwenye makubaliano ya kazi mpaka ufanyaji wake. Siyo mbaya mtu kutumia kipaji chako cha mtaani lakini ukichanganya na suala la emu lazima mtu atakuwa anakeheshimu jinsi ambavyo unaifanya kazi yako" - Nisher aliongeza.

Akizungumzia kuhusu wimbi la waongozaji video kuongezeka kila Siku Nisher amesema "Ma- directors wanavyoongezeka kila siku ni tafsiri ya kuwa industry yetu imekua, suala la kusema huyu hajui siyo tatizo kwa kuwa hata mtoto anapokuwa anakua kuna mambo anakuwa anakosea mpaka anakuwa mtu mzima. Hivyo ma director wachanga nao wakikosea siyo dhambi kwani na wao wanahitaji muda wa  kujifunza zaidi".