Jumamosi , 13th Mar , 2021

Ni headlines za staa wa filamu Wema Sepetu ambaye kupitia mtandao wa Instagram ametangaza kupotelewa kwa mbwa wake na ameahidi kutoa Tsh Milioni 1 kwa atakayeweza kumpata.

Wema Sepetu na Mbwa wake Vanilla

Katika taarifa hiyo Wema Sepetu ameandika kuwa "Mbwa wangu amepotea, kwa yeyote atakayemuona popote please anijulishe kwa namba hii 067974990 na kuna zawadi ya Milioni 1, amepotea asubuhi hii, naomba mnisaidie 'please guys help me' anaitwa Vanilla au Manunu amevaa kigauni cha brown".

Aidha Wema Sepetu aliwahi kusema mbwa wake huyo ndiyo rafiki yake mkubwa na pia anampa mahitaji mengine kama walivyo binaadam kama kumpeleka saloon na kumsafisha.

Tazama interview ya Mzee Kisauji anayetrend kwa kugoma kutoka mitandaoni.