Jumamosi , 6th Mar , 2021

Kulekea siku ya wanawake duniani Machi 8 mwanamke kinara leo ni msanii Gigy Money 'Mama Mayra' ambaye amefunguka kusema uoga wake ndio umemfanya kuwa mtu maarufu.

Msanii Gigy Money

Gigy Money ameshea stori na EATV & EA Radio Digital, kwamba mama yake alimzuia kufanya kazi za sanaa hivyo akaamua kutoa uoga wa kundoka nyumbani kwao hadi sasa amekuwa maarufu utokana na ishu ambazo anazifanya.

"Nilizuliwa na mama yangu kuwa muigizaji, nikaondoka nyumbani kwake na sikurudi, niliona nimekosea tayari na nahisi nilimuonyesha dharau ambayo sijawahi kumfanyia, uoga wangu ukanifanya nizidi kuwa Gigy Money na kuwa mtu maarufu na mama yangu hajui nipo wapi" amesema Gigy Money

#MwanamkeKinara