Jumatano , 18th Jan , 2017

Rapa Roma Mkatoliki ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Usimsahau mchizi' amefunguka na kusema siku zote ukimuona yeye amefanya kazi na Rapa Baghdad basi unachotakiwa ni kuandaa mbavu zako.

Roma na Baghdad

Roma Mkatoliki alisema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo na kudai siku zote wanatoa ngoma kwa lengo ya kuwafurahisha watu, wanatoa ngoma kwa lengo la kufanya watu wacheke na kupunguza stress ndiyo maana kazi hizo wanatoa kila mwezi wa kumi na mbili kipindi ambacho watu wengi wapo likizo.

"Siku zote ukiona Roma na Baghdad wamefanya kazi unachotakiwa kuandaa mbavu zako tu kwani tunafanya kazi kwa lengo la kufurahisha watu, kufanya watu wacheke ndiyo maana kazi zetu za pamoja tunatoa Desemba kipindi ambacho watu wapo likizo lengo watu wafurahi na kupunguza stress za kazi za mwaka mzima" alisema Roma Mkatoliki.

Mbali na hilo Roma Mkatoliki alizungumzia kitendo cha baadhi ya mashabiki kuwachana baada ya kufanya muziki aina ya singeli kwenye wimbo wao wa 'K', Roma anadai kuwa muziki hauna mipaka hivyo mashabiki hawapaswi kumuwekea msanii mipaka ya kufanya kazi, bali msanii anapaswa kuwa huru na kufanya muziki aina yoyote.