Khadija (kushoto) akiwa na kaka yake Mzee Yusuph
Khadija ametoa nyeti hiyo alipokuwa kwenye kipindi cha FNL cha EATV, alipokuwa akifafanua kuhusu madongo anayotupiana na wifi yake huyo, ambapo ilikuwa ikidaiwa kuwa Khadija aliimba wimbo unaomlenga Leila ukimtaarifu kuwa talaka yake iko njiani.
"Sijaongea na Leila miaka mitano, mara ya mwisho nilimsalimia salam Aleykum, lakini hakuitikia, basi, tangu hapo sijaongea naye tena" Alisema Khadija huku akisisiza kuwa hana ugomvi wowote na Leila na kwamba wimbo aliouimba haukumlenga yeye.
Leila ni mke wa Mzee Yusuph kaka wa Khadija Yusuph na tangu Mzee alipotangaza kuacha muziki, pamekuwa na vita ya maneno kati ya mawifi hao, Leila na Khadija, huku kukishuhudiwa kundi la Jahazi Modern Taarab likisambaratika kwa kasi ya aina yake.