Jumatano , 21st Oct , 2020

Mpenzi wa msanii wa filamu Duma Actor aitwaye Mishi Dorah amesema amechambwa sana na watu kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonyesha kuwa yupo kwenye mahaba mazito na msanii huyo wa filamu.

Msanii wa filam Duma na mpenzi wake Mishi Dorah

Mishi Dorah ambaye anatokea Nairobi,Kenya amesema hachoshwi na kelele za watu wa Instagram kwani hazimuumizi kichwa na sasa hivi wapo kwenye mahusiano  kwa miaka mitatu na anaenjoy kuwa na Duma Actor.

"Duma ni 'Gentleman' na ndiyo mwanaume wa ndoto zangu, nilitamani kuwa naye na mtu mzuri sana kwangu, tayari nimeshafika kwao ila nimegundua kuna mawifi wengi na wanachamba sana ila nime-enjoy" amesema Mishi Dorah

Aidha kwa upande wa Duma Actor amesema "Mimi sifanyi kiki kuhusu kupost mitandaoni kama tupo kwenye mahusiano, huyu ni mchumba wangu na mke wangu mtarajiwa, mahusiano yetu yana zaidi ya miaka mitatu tulivyokutana damu zetu zikaendana"