Msanii Zee Cuty upande wa kushoto, kulia ni Uchebe na Shilole
Akizungumzia tukio hilo Zee Cuty mwenyewe amesema kuwa "Mimi na Uchebe tunafahamiana kwenye mazingira ya kazi na alikuwa mume wa dada yangu Shilole ila kuna watu wanadhani nimeingia kwenye kiki na Uchebe, namuheshimu kama mtu ambaye alikuwa na dada yangu, kilichotokea ni salamu tu na nilikuwa nipo kwenye hali ya ujana fulani hivi"
"Nilikuwa namsalimia kawaida sio kama nimemkumbatia vibaya, sikuwaza kama watu watafikiria hivyo na kwa comments zao zimeni-disappoint sana, na sikuwahi kutegemea kama nitakuja kumkwaza dada Shishi kama nimemkosea au amechukia namuomba msamaha, nahisi amejisikia vibaya" ameongeza
Zaidi tazama hapa chini kwenye video.